Hiliyambo limekithiri,alifanyao haoni,
Nalisema nami si siri,limechacha kanisani,
Naona litanawiri,mapema mlikomeni,
Wanadada walokole,tunzeni waume wenu!
Walalama kilamara,eti nyinyi hamweshimu,
Mwajiletea madhara,na pia mwajihukumu,
Wa kanisa ndi vinara,la waume hamweshimu,
Wanadada walokole, tunzeni waume wenu!
Kija kwako mhubiri,kabati walifungua,
Hadi wapanda kwa dari,sahani nzuri watoa,
Mfanyavyo si vizuri,badilisheni tabia,
Wanadada walokole, tunzeni waume wenu!
Wanaume wazunika,Kila muda kanisani,
Nyumbani na waboeka,mfanyapo na kuhani,
Nyoyoni wasononeka,boma lao mabadini,
Wanadada walokole, tunzeni waume wenu!
Wacha mume kafurahi,muishini kwa neema,
Ndoa yenu tamirihi,mtachekelea wema,
Kitazama tanabahi,mtasifiwa salama,
Wanadada walokole, tunzeni waume wenu!
Safari nazo punguza,mrembeshe wako mume,
Najua nimewaguza,mume siye paka shume,
Yeye atauguuza, moyo wako usikwame,
Wanadada walokole, tunzeni waume wenu!
Rekebisheni nasihi,ndoa ziache vunjika,
Someni wangu nasihi, mbeleni nawapeleka,
Nasaha Nimewaahi,ndoa na hazitavunjika,
Wanadada walokole, tunzeni waume wenu!
|Wanadada walokole|
-